Kikao cha DSFA na Mawakala wa Meli za Uvuvi
Kikao cha DSFA na Mawakala wa Meli za Uvuvi
Imewekwa: 19 June, 2024
Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) imefanya kikao na Mawakala wa meli za uvuvi Tanzania na kutoa uelewa juu ya masuala ya sheria, takwimu, leseni pamoja na udhibiti. Kikao hicho kilifunguliwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu Dkt. Saleh A. Yahya kilichofanyika katika ukumbi wa jengo la Mvuvi House jijini Dar es Salaam.